31Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.