16 Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,