12 Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.