Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 6:21-35 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 6:21-35 in Biblia ya Kiswahili

21 Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.
Mithali 6 in Biblia ya Kiswahili