Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 5:2-12 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 5:2-12 in Biblia ya Kiswahili

2 ili ujifunze busara na midomo yako iweze kuhifadhi maarifa.
3 Maana midomo ya malaya hutiririsha asali na kinywa chake ni laini kuliko mafuta,
4 lakini mwishoni anakuwa mchungu kama mnyoo, hukata kama upunga mkali.
5 Miguu yake huelekea mauti; hatua zake huelekea njia yote ya kuzimu.
6 Hafikirii njia ya uzima. Hatua za miguu yake hupotea, maana hajui anakwenda wapi.
7 Sasa, wanangu, nisikilizeni; wala msiache kusikiliza maneno ya kinywa changu.
8 Lindeni njia yenu mbali naye wala msiende karibu na mlango wa nyumba yake.
9 Kwa njia hiyo hamtawapa wengine heshima yenu au miaka ya uzima wenu kwa mtu mkatiri;
10 wageni usije kufanya karamu kwa utajiri wenu; kazi mliyoifanya haitaenda katika nyumba ya wageni.
11 Mwishoni mwa maisha yenu mtajuta ambapo nyama na mwili wenu vitaangamia.
12 Nanyi mtasema, “Namna gani nilichukia fundisho na moyo wangu ulidharau sahihisho!
Mithali 5 in Biblia ya Kiswahili