Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 4:6-16 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 4:6-16 in Biblia ya Kiswahili

6 usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
7 Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
8 Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
9 Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
10 Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
11 Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12 Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
13 Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
14 Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
15 Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
16 Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
Mithali 4 in Biblia ya Kiswahili