Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 3:4-22 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 3:4-22 in Biblia ya Kiswahili

4 Ndipo utapata kibali na heshima mbele Mungu na wanadamu.
5 Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote na wala usitegemee ufahamu wako mwenyewe,
6 katika njia zako zote mkiri Yeye na yeye atayanyosha mapito yako.
7 Usiwe mwenye busara machoni pako mwenyewe; mche Yehova na jiepushe na uovu.
8 Itakuponya mwili wako na kukuburudisha mwili wako.
9 Mheshimu Yehova kwa utajiri wako na kwa malimbuko ya mazao kwa kila unachozalisha,
10 na ndipo ghala zako zitajaa na mapipa makubwa yatafurika kwa divai mpya.
11 Mwanangu, usidharau kuadibishwa na Yohova na wala usichukie karipio lake,
12 maana Yehova huwaadibisha wale wapendao, kama baba anavyoshughulika kwa mtoto wake ampendezaye.
13 Yeye apataye hekima anafuraha, naye hupata ufahamu.
14 Kwani katika hekima unapata manufaa kuliko ukibadilisha kwa fedha na faida yake inafaa zaidi kuliko dhahabu.
15 Hekima inathamani zaidi kuliko kito, na hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na hekima.
16 Yeye anasiku nyingi katika mkono wake wa kuume; na mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima.
17 Njia zake ni njia za ukarimu na mapito yake ni amani.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomshikilia, wale wanaomshikilia wanafuraha.
19 Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu.
20 Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake.
21 Mwanangu, zingatia hukumu ya kweli na ufahamu, na wala usiache kuvitazama.
22 Vitakuwa uzima wa nafsi yako na urembo wa hisani wa kuvaa shingoni mwako.
Mithali 3 in Biblia ya Kiswahili