26 kwa maana Yehova utakuwa upande wako na ataulinda mguu wako usinaswe kwenye mtego.
27 Usizuie mema kwa wale wanaoyastahili, wakati utendaji upo ndani ya mamlaka yako.
28 Jirani yako usimwambie, “Nenda, na uje tena, na kesho nitakupa,” wakati pesa unazo.
29 Usiweke mpango wa kumdhuru jirani yako- anayeishi jirani nawe na yeye anakuamini.
30 Usishindane na mtu pasipo sababu, ikiwa hajafanya chochote kukudhuru.
31 Usimhusudu mtu jeuri au kuchagua njia zake zozote.
32 Maana mtu mjanja ni chukizo kwa Yehova, bali humleta mtu mwaminifu kwenye tumaini lake.