Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 3:2-16 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 3:2-16 in Biblia ya Kiswahili

2 maana ziatakuongezea siku zako na miaka ya maisha yako na amani.
3 Usiache utiifu wa agano na uaminifu viondoke kwako, vifunge katika shingo yako, viandike katika vibao vya moyo wako.
4 Ndipo utapata kibali na heshima mbele Mungu na wanadamu.
5 Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote na wala usitegemee ufahamu wako mwenyewe,
6 katika njia zako zote mkiri Yeye na yeye atayanyosha mapito yako.
7 Usiwe mwenye busara machoni pako mwenyewe; mche Yehova na jiepushe na uovu.
8 Itakuponya mwili wako na kukuburudisha mwili wako.
9 Mheshimu Yehova kwa utajiri wako na kwa malimbuko ya mazao kwa kila unachozalisha,
10 na ndipo ghala zako zitajaa na mapipa makubwa yatafurika kwa divai mpya.
11 Mwanangu, usidharau kuadibishwa na Yohova na wala usichukie karipio lake,
12 maana Yehova huwaadibisha wale wapendao, kama baba anavyoshughulika kwa mtoto wake ampendezaye.
13 Yeye apataye hekima anafuraha, naye hupata ufahamu.
14 Kwani katika hekima unapata manufaa kuliko ukibadilisha kwa fedha na faida yake inafaa zaidi kuliko dhahabu.
15 Hekima inathamani zaidi kuliko kito, na hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na hekima.
16 Yeye anasiku nyingi katika mkono wake wa kuume; na mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima.
Mithali 3 in Biblia ya Kiswahili