Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 3:19-30 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 3:19-30 in Biblia ya Kiswahili

19 Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu.
20 Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake.
21 Mwanangu, zingatia hukumu ya kweli na ufahamu, na wala usiache kuvitazama.
22 Vitakuwa uzima wa nafsi yako na urembo wa hisani wa kuvaa shingoni mwako.
23 Ndipo utatembea katika njia yako kwa usalama na mguu wako hautajikwaa;
24 ulalapo hutaogopa; utakapolala, usingizi wako utakuwa mtamu.
25 Usitishwe na hofu ya ghafula au uharibifu uliosababishwa na waovu unapotokea,
26 kwa maana Yehova utakuwa upande wako na ataulinda mguu wako usinaswe kwenye mtego.
27 Usizuie mema kwa wale wanaoyastahili, wakati utendaji upo ndani ya mamlaka yako.
28 Jirani yako usimwambie, “Nenda, na uje tena, na kesho nitakupa,” wakati pesa unazo.
29 Usiweke mpango wa kumdhuru jirani yako- anayeishi jirani nawe na yeye anakuamini.
30 Usishindane na mtu pasipo sababu, ikiwa hajafanya chochote kukudhuru.
Mithali 3 in Biblia ya Kiswahili