Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 31:15-31 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 31:15-31 in Biblia ya Kiswahili

15 Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
16 Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
17 Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
18 Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
19 Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
20 Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
21 Haogopi theluji kwa ajili ya kaya yake, kwa maana nyumba yake yote imevika kwa nguo nyekundu.
22 Hutengeneza matandiko ya kitanda chake, na huvaa nguo za kitani ya dhambarau safi.
23 Mume wake anajulikana malangoni, anapoketi na wazee wa nchi.
24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, na naleta mishipi kwa wafanyabiashara.
25 Amevaa nguvu na heshima, na wakati ujao huucheka.
26 Anafumbua kinywa chake kwa hekima na sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake.
27 Huangalia njia za nyumba yake na hawezi kula mkate wa uvivu.
28 Watoto wake huinuka na kumwita heri na mume wake humsifia, akisema,
29 “Wanawake wengi wamefanya vizuri, lakini wewe umewapita wote.”
30 Madaha ni udanganyifu, uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Yehova, atasifiwa.
31 Mpeni tunda la mikono yake na kazi zake zimsifu katika malango.
Mithali 31 in Biblia ya Kiswahili