Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 30:16-27 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 30:16-27 in Biblia ya Kiswahili

16 Kuzimu, tumbo tasa, nchi yenye kiu kwa maji, na moto usiosema, “Inatosha.”
17 Jicho ambalo linamdhihaki baba na kudharau utii kwa mama, macho yake yatadonolewa na kunguru wa bondeni, na ataliwa na tai.
18 Kuna vitu vitatu ambavyo vinanishangaza, vinne ambavyo sivifahamu:
19 njia ya tai angani; njia ya nyoka juu ya mwamba; njia ya meli kwenye moyo wa bahari; na njia ya mtu pamoja mwanake kijana.
20 Hii ni njia ya mzinzi- anakula na kufuta kinywa chake na kusema, “sijafanya ubaya wowote.”
21 Chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka na vinne haiwezi kuvivumilia:
22 mtumwa anapokuwa mfalme; mpumbavu anaposhiba vyakula;
23 mwanamke anayechukiwa anapoolewa; kijakazi anapochukua nafasi ya mkuu wake.
24 Vitu vinne duniani ni vidogo na bado vinabusara:
25 mchwa ni viumbe ambao sio imara, lakini huandaa chakula chao wakati wa hari,
26 Wibari siyo viumbe wenye nguvu, lakini hutengeneza makazi yake kwenye miamba.
27 Nzige hawana mfalme, lakini wote wanamwendo wa mpangilio.
Mithali 30 in Biblia ya Kiswahili