Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 30

Mithali 30:16-27

Help us?
Click on verse(s) to share them!
16Kuzimu, tumbo tasa, nchi yenye kiu kwa maji, na moto usiosema, “Inatosha.”
17Jicho ambalo linamdhihaki baba na kudharau utii kwa mama, macho yake yatadonolewa na kunguru wa bondeni, na ataliwa na tai.
18Kuna vitu vitatu ambavyo vinanishangaza, vinne ambavyo sivifahamu:
19njia ya tai angani; njia ya nyoka juu ya mwamba; njia ya meli kwenye moyo wa bahari; na njia ya mtu pamoja mwanake kijana.
20Hii ni njia ya mzinzi- anakula na kufuta kinywa chake na kusema, “sijafanya ubaya wowote.”
21Chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka na vinne haiwezi kuvivumilia:
22mtumwa anapokuwa mfalme; mpumbavu anaposhiba vyakula;
23mwanamke anayechukiwa anapoolewa; kijakazi anapochukua nafasi ya mkuu wake.
24Vitu vinne duniani ni vidogo na bado vinabusara:
25mchwa ni viumbe ambao sio imara, lakini huandaa chakula chao wakati wa hari,
26Wibari siyo viumbe wenye nguvu, lakini hutengeneza makazi yake kwenye miamba.
27Nzige hawana mfalme, lakini wote wanamwendo wa mpangilio.

Read Mithali 30Mithali 30
Compare Mithali 30:16-27Mithali 30:16-27