Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 2:6-13 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 2:6-13 in Biblia ya Kiswahili

6 Kwa kuwa Yohova hutoa hekima, katika kinywa chake hutoka maarifa na ufahamu.
7 Yeye huhifadhi sauti ya hekima kwa wale wampendezao, yeye ni ngao kwa wale waendao katika uadilifu,
8 huongoza katika njia za haki na atalinda njia ya waaminifu kwake.
9 Ndipo utakapoelewa wema, haki, usawa na kila njia njema.
10 Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11 Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
12 Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
13 Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
Mithali 2 in Biblia ya Kiswahili