Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 26:1-9 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 26:1-9 in Biblia ya Kiswahili

1 Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2 Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3 Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4 Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5 Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6 Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7 Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8 Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9 Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
Mithali 26 in Biblia ya Kiswahili