4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.