22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.