17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,