Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 24:16-22 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 24:16-22 in Biblia ya Kiswahili

16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
Mithali 24 in Biblia ya Kiswahili