2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.