2Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
3Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.