Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 20:8-22 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 20:8-22 in Biblia ya Kiswahili

8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Mithali 20 in Biblia ya Kiswahili