Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 20:3-15 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 20:3-15 in Biblia ya Kiswahili

3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Mithali 20 in Biblia ya Kiswahili