18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?