7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
8 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
9 Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
10 Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
11 Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
12 Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.