Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 16:3-9 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 16:3-9 in Biblia ya Kiswahili

3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
Mithali 16 in Biblia ya Kiswahili