Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 16:24-32 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 16:24-32 in Biblia ya Kiswahili

24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
Mithali 16 in Biblia ya Kiswahili