Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 15:19-29 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 15:19-29 in Biblia ya Kiswahili

19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu.
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
Mithali 15 in Biblia ya Kiswahili