Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 11:13-21 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 11:13-21 in Biblia ya Kiswahili

13 Anayekwenda akizunguka kwa kukashifu hufunua siri, bali mtu mwaminifu hustiri jambo.
14 Pasipokuwa na uongozi wenye busara, taifa huanguka, bali ushindi huja kwa kushauriana washauri wengi.
15 Anayemdhamini mkopo wa mgeni ataumia kwa usumbufu, bali anayechukia kutoa rehani kwa namna ya ahadi yupo salama.
16 Mwanamke mwenye rehema hupata heshima, bali watu wakorofi hufumbata utajiri.
17 Mtu mkarimu hufaidika mwenyewe, bali mkatili hujiumiza mwenyewe.
18 Mtu mwovu husema uongo kupata mishahara yake, bali yeye apandaye haki anavuna mishahara ya kweli.
19 Mtu mwaminifu atendaye haki ataishi, bali yeye atendaye uovu atakufa.
20 Yehova anawachukia wenye ukaidi mioyoni, bali anawapenda wale ambao njia zao hazina makosa.
21 Uwe na uhakika juu ya hili- watu waovu hawatakosa adhabu, bali uzao wa wale watendao haki watawekwa salama.
Mithali 11 in Biblia ya Kiswahili