Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 11

Mithali 11:13-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Anayekwenda akizunguka kwa kukashifu hufunua siri, bali mtu mwaminifu hustiri jambo.
14Pasipokuwa na uongozi wenye busara, taifa huanguka, bali ushindi huja kwa kushauriana washauri wengi.
15Anayemdhamini mkopo wa mgeni ataumia kwa usumbufu, bali anayechukia kutoa rehani kwa namna ya ahadi yupo salama.
16Mwanamke mwenye rehema hupata heshima, bali watu wakorofi hufumbata utajiri.
17Mtu mkarimu hufaidika mwenyewe, bali mkatili hujiumiza mwenyewe.
18Mtu mwovu husema uongo kupata mishahara yake, bali yeye apandaye haki anavuna mishahara ya kweli.
19Mtu mwaminifu atendaye haki ataishi, bali yeye atendaye uovu atakufa.
20Yehova anawachukia wenye ukaidi mioyoni, bali anawapenda wale ambao njia zao hazina makosa.
21Uwe na uhakika juu ya hili- watu waovu hawatakosa adhabu, bali uzao wa wale watendao haki watawekwa salama.

Read Mithali 11Mithali 11
Compare Mithali 11:13-21Mithali 11:13-21