Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mhubiri 7:15-24 in Swahili (individual language)

Help us?

Mhubiri 7:15-24 in Biblia ya Kiswahili

15 Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
16 Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
17 Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
18 Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
19 Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
20 Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
21 Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.
22 Vivyo hivyo unafahamu mwenyewe ndani ya moyo wako umewalaani wengine mara kadhaa.
23 Haya yote nimeyathibitisha kwa hekima. Nikasema, “nitakuwa mwenye hekima,” lakini zaidi ambavyo ningekuwa.
24 Hekima i mbali na kina sana. Ni nani awezaye kuipata?
Mhubiri 7 in Biblia ya Kiswahili