Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mambo ya Walawi - Mambo ya Walawi 18

Mambo ya Walawi 18:6-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
6Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.

Read Mambo ya Walawi 18Mambo ya Walawi 18
Compare Mambo ya Walawi 18:6-15Mambo ya Walawi 18:6-15