Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Luka 2:47-51 in Swahili (individual language)

Help us?

Luka 2:47-51 in Biblia Takatifu

47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
Luka 2 in Biblia Takatifu

Luka 2:47-51 in Biblia ya Kiswahili

47 Wote waliomsikia walishangazwa na ufahamu wake na majibu yake.
48 Walipomwona, walistaajabu. Mama yake akamwambia, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivi? Sikiliza, baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa.”
49 Akawaambia, “Kwa nini mmekuwa mkinitafuta? Hamkujua kwamba lazima niwe kwenye nyumba ya Baba yangu?
50 Lakini hawakuelewa nini alichomaanisha kwa maneno hayo.
51 Ndipo akaenda pamoja nao mpaka nyumbani Nazareti na alikuwa mtii kwao. Mama yake alihifadhi mambo yote moyoni mwake.
Luka 2 in Biblia ya Kiswahili