40Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
41Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
42Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
43Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”