Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Hesabu 13:3-16 in Swahili (individual language)

Help us?

Hesabu 13:3-16 in Biblia ya Kiswahili

3 Musa akawatuma kutoka jangwa la Parani, ili watii amri ya BWANA. Watu wote hao walikuwa viongozi wa watu wa Israeli.
4 Majina yao yalikuwa haya yafuatayo: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 Kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
8 Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
10 kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
11 kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
13 kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
15 kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
16 Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
Hesabu 13 in Biblia ya Kiswahili