Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 94:3-11 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 94:3-11 in Biblia ya Kiswahili

3 Mpaka lini waovu, Yahwe, mpaka lini waovu watafurahia?
4 Wanamwaga maneno yao ya kiburi; wote watendao uovu wanajivuna.
5 Wanawaangamiza watu wako, Yahwe; wanalitesa taifa ambao ni milki yako.
6 Wanamuua mjane na mgeni aishiye nchini mwao, na wanamuua yatima.
7 Nao husema, “Yahwe hawezi kuona, Mungu wa Yakobo hayagundui haya.”
8 Tambueni, ninyi watu wajinga! Enyi wapumbavu, mtajifunza lini?
9 Yeye aliye liumba sikio, hasikii? Yeye aliye litengeneza jicho, haoni?
10 Yeye awaadhibuye mataifa, hayuko sahihi? Yeye ndiye ampaye maarifa mwanadamu.
11 Yahwe anayajua mawazo ya wanadamu, kuwa ni mvuke.
Zaburi 94 in Biblia ya Kiswahili