3 Mpaka lini waovu, Yahwe, mpaka lini waovu watafurahia?
4 Wanamwaga maneno yao ya kiburi; wote watendao uovu wanajivuna.
5 Wanawaangamiza watu wako, Yahwe; wanalitesa taifa ambao ni milki yako.
6 Wanamuua mjane na mgeni aishiye nchini mwao, na wanamuua yatima.
7 Nao husema, “Yahwe hawezi kuona, Mungu wa Yakobo hayagundui haya.”
8 Tambueni, ninyi watu wajinga! Enyi wapumbavu, mtajifunza lini?
9 Yeye aliye liumba sikio, hasikii? Yeye aliye litengeneza jicho, haoni?
10 Yeye awaadhibuye mataifa, hayuko sahihi? Yeye ndiye ampaye maarifa mwanadamu.
11 Yahwe anayajua mawazo ya wanadamu, kuwa ni mvuke.