Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 94:2-14 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 94:2-14 in Biblia ya Kiswahili

2 Inuka, muhukumu wa nchi, uwape wenye majivuno kile wanachosahili.
3 Mpaka lini waovu, Yahwe, mpaka lini waovu watafurahia?
4 Wanamwaga maneno yao ya kiburi; wote watendao uovu wanajivuna.
5 Wanawaangamiza watu wako, Yahwe; wanalitesa taifa ambao ni milki yako.
6 Wanamuua mjane na mgeni aishiye nchini mwao, na wanamuua yatima.
7 Nao husema, “Yahwe hawezi kuona, Mungu wa Yakobo hayagundui haya.”
8 Tambueni, ninyi watu wajinga! Enyi wapumbavu, mtajifunza lini?
9 Yeye aliye liumba sikio, hasikii? Yeye aliye litengeneza jicho, haoni?
10 Yeye awaadhibuye mataifa, hayuko sahihi? Yeye ndiye ampaye maarifa mwanadamu.
11 Yahwe anayajua mawazo ya wanadamu, kuwa ni mvuke.
12 Amebarikiwa yule ambaye umuongozaye, Yahwe, yule ambaye wewe humfundisha kutoka katika sheria yako.
13 Wewe humpa pumziko wakati wa shida mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya waovu.
14 Maana Yahwe hatawaacha watu wake wala kutelekeza warithi wake.
Zaburi 94 in Biblia ya Kiswahili