Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 92:4-12 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 92:4-12 in Biblia ya Kiswahili

4 Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
5 Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
6 Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
7 Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
8 Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
9 Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
10 Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
11 Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
12 Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
Zaburi 92 in Biblia ya Kiswahili