Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 90:1-10 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 90:1-10 in Biblia ya Kiswahili

1 Bwana, wewe umekuwa kimbilio letu vizazi vyote.
2 Kabla milima haijaumbwa, wala haujaumba nchi na dunia, tangu milele na milele, wewe ni Mungu.
3 Humrudisha mtu mavumbini, na kusema, “Rudi, ewe uzao wa mwanadmu.
4 Kwa maana miaka elfu machoni pako ni kama jana ipitapo, na kama saa wakati wa usiku.
5 Huwafagia kama vile kwa mafuliko nao hulala; na wakati wa asubuhi wako kama majani yameayo.
6 Asubuhi yachipuka na kumea; jioni yakatika na kukauka.
7 Hakika, tumeangamizwa kwa hasira yako, na gadhabu yako inatuogopesha sana.
8 Umeudhihirisha uovu wetu mbele zako, na dhambi zetu zilizofichika katika nuru ya uwepo wako.
9 Uhai wetu unatoweka chini ya gadhabu yako; Miaka yetu inapita haraka kama pumzi.
10 Miaka yetu ni sabini, au themanini tukiwa na afya; lakini hata hivyo miaka yetu mizuri imetiwa alama ya taabu na huzuni. Ndiyo, inapita haraka, kisha tunatoweka.
Zaburi 90 in Biblia ya Kiswahili