Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 89:6-13 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 89:6-13 in Biblia ya Kiswahili

6 Maana ni nani katika mbingu aweza kulinganishwa na Yahwe? Ambaye kati ya wana wa miungu ni kama Yahwe?
7 Ni Mungu anaye heshimiwa sana katika baraza la watakatifu naye ni wakutisha kati ya wote wanao mzunguka.
8 Yahwe, Mungu wa majeshi, ni nani aliye na nguvu kama wewe, Yahwe? Kweli yako inakuzunguka.
9 Wewe huitawala bahari yenye nguvu; mawimbi yainukapo, wewe huyatuliza.
10 Ulimwangamiza Rahabu kama mmoja aliye uliwa. Uliwatawanya adui zako kwa mkono wako wenye nguvu.
11 Mbingu ni zako wewe, na nchi pia. Uliiumba dunia na vyote vilivyomo.
12 Uliumba kaskazini na kusini. Tabori na Hermoni hulifurahia jina lako.
13 una mkono wa uweza na mkono wenye nguvu, na mkono wako wa kuume uko juu.
Zaburi 89 in Biblia ya Kiswahili