Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 89:33-43 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 89:33-43 in Biblia ya Kiswahili

33 Lakini sitauondoa kwake upendo wangu thabiti wala kutokuwa mwaminifu kwa ahadi yangu.
34 Sitavunja agano langu wala kubadilisha maneno ya midomoni mwangu.
35 Mara moja na kwa yote, nimeapa kwa utakatifu wangu sitamdanganya Daudi:
36 uzao wake utaendelea milele na kiti chake cha enzi kama vile jua mbele yangu.
37 Kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu mawinguni.” Selah
38 Lakini wewe umemtupa na kumkataa; umemkasirikia mfalme mpakwa mafuta wako.
39 Wewe umelikataa agano la mtumishi wako. Umeinajisi taji yake ardhini.
40 Umevunja kuta zake zote. Umeharibu ngome yake.
41 Wapita njia wote wamemuibia, amekuwa kitu chenye kinyaa kwa majirani zake.
42 Umeinua mkono wa kuume wa adui zake; umewafurahisha adui zake wote.
43 Umeyageuza makali ya upanga wake. Na hukumfanya asimame awapo vitani.
Zaburi 89 in Biblia ya Kiswahili