Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 89:29-40 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 89:29-40 in Biblia ya Kiswahili

29 Nitaufanya uzao wake kudumu milele na kiti chake cha enzi kitadumu kama mbingu zilizo juu.
30 Ikiwa watoto wake wataziacha sheria zangu na kutokutii amri zangu,
31 na kama watazivunja sheria zangu na kutokuzishika amri zangu,
32 ndipo nitauadhiu uasi wao kwa fimbo na uovu wao kwa makofi.
33 Lakini sitauondoa kwake upendo wangu thabiti wala kutokuwa mwaminifu kwa ahadi yangu.
34 Sitavunja agano langu wala kubadilisha maneno ya midomoni mwangu.
35 Mara moja na kwa yote, nimeapa kwa utakatifu wangu sitamdanganya Daudi:
36 uzao wake utaendelea milele na kiti chake cha enzi kama vile jua mbele yangu.
37 Kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu mawinguni.” Selah
38 Lakini wewe umemtupa na kumkataa; umemkasirikia mfalme mpakwa mafuta wako.
39 Wewe umelikataa agano la mtumishi wako. Umeinajisi taji yake ardhini.
40 Umevunja kuta zake zote. Umeharibu ngome yake.
Zaburi 89 in Biblia ya Kiswahili