Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 89:27-35 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 89:27-35 in Biblia ya Kiswahili

27 Nitamjalia kuwa kama mzaliwa wangu wa kwanza, aliye inuliwa zaidi juu ya wafalme wa nchi.
28 Nitaongeza uaminifu wa agano langu kwake milele; na agano langu pamoja naye litakuwa salama.
29 Nitaufanya uzao wake kudumu milele na kiti chake cha enzi kitadumu kama mbingu zilizo juu.
30 Ikiwa watoto wake wataziacha sheria zangu na kutokutii amri zangu,
31 na kama watazivunja sheria zangu na kutokuzishika amri zangu,
32 ndipo nitauadhiu uasi wao kwa fimbo na uovu wao kwa makofi.
33 Lakini sitauondoa kwake upendo wangu thabiti wala kutokuwa mwaminifu kwa ahadi yangu.
34 Sitavunja agano langu wala kubadilisha maneno ya midomoni mwangu.
35 Mara moja na kwa yote, nimeapa kwa utakatifu wangu sitamdanganya Daudi:
Zaburi 89 in Biblia ya Kiswahili