Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 89:21-34 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 89:21-34 in Biblia ya Kiswahili

21 Mkono wangu utamsaidia yeye; mkono wangu utamtia nguvu.
22 Hakuna adui atakaye mdanganya; hakuna mwana wa uovu atakaye muonea.
23 Nitawaangamiza adui zake mbele yake; nitawaua wale wamchukiao.
24 Kweli yangu na uaminifu wa agano vitakuwa pamoja naye; kupitia jina langu atakuwa mshindi.
25 Nitaweka mkono wake juu ya bahari na mkono wake wa kuume juu ya mito.
26 Yeye ataniita, 'Wewe ni Baba yangu, Mungu wangu, na mwamba wa wokovu wangu.'
27 Nitamjalia kuwa kama mzaliwa wangu wa kwanza, aliye inuliwa zaidi juu ya wafalme wa nchi.
28 Nitaongeza uaminifu wa agano langu kwake milele; na agano langu pamoja naye litakuwa salama.
29 Nitaufanya uzao wake kudumu milele na kiti chake cha enzi kitadumu kama mbingu zilizo juu.
30 Ikiwa watoto wake wataziacha sheria zangu na kutokutii amri zangu,
31 na kama watazivunja sheria zangu na kutokuzishika amri zangu,
32 ndipo nitauadhiu uasi wao kwa fimbo na uovu wao kwa makofi.
33 Lakini sitauondoa kwake upendo wangu thabiti wala kutokuwa mwaminifu kwa ahadi yangu.
34 Sitavunja agano langu wala kubadilisha maneno ya midomoni mwangu.
Zaburi 89 in Biblia ya Kiswahili