Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 89:13-29 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 89:13-29 in Biblia ya Kiswahili

13 una mkono wa uweza na mkono wenye nguvu, na mkono wako wa kuume uko juu.
14 Haki na hukumu ni msingi wa kiti chako. Uaminifu wa agano lako na uaminifu huja mbele zako.
15 Wamebarikiwa watu wakuabuduo wewe! Yahwe, wanatembea katika nuru ya uso wako.
16 Siku zote wanafurahia katika jina lako, na katika haki yako wanakutukuza wewe.
17 Wewe ni fahari ya nguvu zao, na kwa nguvu zako tu washindi.
18 Maana ngao zetu ni za kwako Yahwe; mfalme wetu ni wa Mtakatifu wa Israeli.
19 Muda mrefu uliopita ulizungumza na waaminfu wako katika maono; ulisema, “Nimeweka taji juu ya mwenye nguvu; nimemuinua aliyechaguliwa kutoka kati ya watu.
20 Nimemchagua Daudi mtumishi wangu; kwa mafuta yangu matakatifu nimempaka yeye.
21 Mkono wangu utamsaidia yeye; mkono wangu utamtia nguvu.
22 Hakuna adui atakaye mdanganya; hakuna mwana wa uovu atakaye muonea.
23 Nitawaangamiza adui zake mbele yake; nitawaua wale wamchukiao.
24 Kweli yangu na uaminifu wa agano vitakuwa pamoja naye; kupitia jina langu atakuwa mshindi.
25 Nitaweka mkono wake juu ya bahari na mkono wake wa kuume juu ya mito.
26 Yeye ataniita, 'Wewe ni Baba yangu, Mungu wangu, na mwamba wa wokovu wangu.'
27 Nitamjalia kuwa kama mzaliwa wangu wa kwanza, aliye inuliwa zaidi juu ya wafalme wa nchi.
28 Nitaongeza uaminifu wa agano langu kwake milele; na agano langu pamoja naye litakuwa salama.
29 Nitaufanya uzao wake kudumu milele na kiti chake cha enzi kitadumu kama mbingu zilizo juu.
Zaburi 89 in Biblia ya Kiswahili