Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 84:6-12 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 84:6-12 in Biblia ya Kiswahili

6 Wanapopita katika bonde la machozi, hupata chemchem ya maji kwa ajili ya kunywa. Mvua ya vuli hulivika baraka.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu; kila mmoja wao katika sayuni huonekana mbele ya Mungu.
8 Yahwe Mungu wa majeshi, sikia maombi yangu; Mungu wa Yakobo, usikilize nisemacho! Selah
9 Ee Mungu, uiangalie ngao yetu; uwaangalie wapakwa mafuta wako.
10 Kwa maana siku moja katika nyumba yako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine. Ni bora niwe mlinzi wa mlango katika nyumba ya Mungu wangu, kuliko kuishi katika mahema ya waovu.
11 Kwa kuwa Yahwe Mungu ni jua letu na ngao yetu; Yahwe atatoa neema na utukufu; hazuii zuri lolote kwa wale ambao hutembea katika uadilifu.
12 Yahwe wa majeshi, amebarikiwa mtu yule anaye kutumainia wewe.
Zaburi 84 in Biblia ya Kiswahili