9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.