Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 83:6-15 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 83:6-15 in Biblia ya Kiswahili

6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
Zaburi 83 in Biblia ya Kiswahili