64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.