Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 78:58-68 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 78:58-68 in Biblia ya Kiswahili

58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Zaburi 78 in Biblia ya Kiswahili